Header Ads


KOREA KASKAZINI YARUSHA KOMBORA JINGINE




Maafisa wa kijeshi nchini Korea Kusini wanasema Korea Kaskazini imejaribu kurusha kombora kutoka kwa manowari ya kivita na kukiuka vikwazo vya kimataifa
Wanasema kuwa kombora hilo hatahivyo lilifeli muda mfupi baada ya kurushwa


Urushaji huo wa kombora unajiri baada ya Korea Kusini na Marekani kukubaliana kuweka mitambo ya kujikinga dhidi ya makombora nchini Korea Kusini.


Nchi hizo mbili ziliafikia mpango huo baada ya majaribio kadha ya makombora yaliyofanywa na Korea Kaskazini mapema mwaka huu.

No comments

Powered by Blogger.