Header Ads


KILO 48 ZA MADAWA YA KULEVYA ZATEKETEZWA TANGA


 Mahakama kuu kanda ya Tanga imeteketeza dawa za kulevya aina ya ''heroin''kilogram 48.3 zilizokuwa na thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 2.4 baada ya Mahakama hiyo kujiridhisha kutoka kwa mkemia wa serikali.
Dawa hizo zimeteketezwa katika tanuru la kiwanda cha kutengeneza saruji cha Rhino kilichopo jijini Tanga chini ya ulinzi mkali wa polisi na kushuhudiwa na wanasheria walikiongozwa na jaji wa Mahakama kuu kanda ya Tanga mheshimiwa Upendo Msuya.
 
Akizungumza baada ya kuteketezwa kwa dawa hizo Mkurugenzi wa mashtaka nchini (DPP) Biswalo maganga amesema dawa hizo zilikamatwa Oktoba 09/2010 katika kizuizi cha Jeshi la Polisi kilichopo eneo la Kabuku mkoani tanga yakitokea jijini Dar es Salaam yakiwahusisha raia wawili watanzania Ismail Sheb Aslam na Rashid Said salim pamoja na raia mmoja kutoka Iran Majid Ardmand ambao wote kwa pamoja wapo mahabusu huku shauri lao likiendelea kusikilizwa.
 
Hili ni tukio la pili la kuteketezwa kwa shehena ya dawa za kulevya aina ya heroin ambapo awali shauri kama hilo lilimhusisha Bakari Kileo Bakari ambaye inadaiwa kuwa alikamatwa na kilo 90 za dawa za kulevya na kutiwa hatiani na Mahakama kuu kanda ya Tanga kisha kuhukumiwa kwenda jela miaka 25.

No comments

Powered by Blogger.