INDIA YAANZISHA WIZARA YA FURAHA YAANI "MINISTRY OF HAPPYNESS"
Kuwa na furaha na amani katika maisha kunachangia maendeleo kwa kiasi kikubwa kulinganisha na pale ambapo vyote hivyo vinapokosekana. Hivyo serikali ya Indiaimeamua kuanzisha wizara itakayo simamia na kuhakikisha wananchi wake wanakua na furaha yaani “MINISTRY OF HAPPYNESS”.
Ambapo serikali hiyo imetangaza kuwa wizara hiyo ya furaha itakuwa na majukumu ya kuhakikisha wananchi wanakua na furaha ambapo pia itakuwa inawashauri ni namna gani wanaweza kuishi vizuri na kwa furaha siku zote. Pia itasisitiza juu ya kufanya mazoezi ya ku relax “YOGA” mafundisho ya kiroho ili kupunguza msongo wa mawazo.
Jimbo la Mandya Pradesh ambapo ndipo idea ama wazo lilipozinduliwa, ni moja kati ya maeneo ambayo maendeleo sio makubwa nchini India na kuna kiwango kikubwa cha mauaji binafsi kwa watoto na wakulima kutokana na ugumu wa maisha.
Licha ya hayo yote pia jimbo hilo lililopo katikati ya India linaongoza kwa mauaji ya watoto wachanga na matukio ya ubakaji. Serikali ya India inaamini kwa kuanzisha wizara ya furaha, haya yote yatapungua.
Post a Comment