Header Ads


MUSEVENI AKAA BARABARANI KUPOKEA SIMU



Rais wa Uganda Bw Yoweri Kaguta Museveni alizua kioja katika kijiji cha Kyeirumba, wilaya ya Isingiro karibu na mpaka wa Uganda na Tanzania aliposimamisha msafara wake wa magari ili apokee simu "ya dharura". Picha za kisa hicho zilipakiwa kwenye mtandao wa Facebook na afisa wake wa habari Don Wanyama.
Amini usiamini Rais Yoweri Museveni, alishuka kutoka kwenye gari lake rasmi akachukua kiti chake na kukiweka kando kando ya barabara mpya ya Isingiro ikipitia kijiji hicho cha Kyeirumba hadi Tanzania na kupokea simu faraghani.





Ilikuwa ajabu sana kwao kumuona Museveni akiwa ameketi barabarani.
Waganda katika mitandao ya kijamii wamesambaza picha hiyo ya rais museveni akizungumza kwa simu ambayo inaonekana kuwa sio ya kisasa.




Ilikuwa ajabu sana kwao kumuona Museveni akiwa ameketi barabarani.
Waganda katika mitandao ya kijamii wamesambaza picha hiyo ya rais museveni akizungumza kwa simu ambayo inaonekana kuwa sio ya kisasa.




Wengine wanamkejeli kwa kuhofia kudukuliwa huku wengine wakimkosoaa kwa kuketi barabarani.
''Kwani hangeweza kupokea simu yake ndani ya gari lake?"
''Ni siri gani hiyo ambayo hakutaka hata walinzi wake wasikie.
''Ama ilikuwa ni #Besigyexit?", wakizungumzia kuachiliwa kwa dhamana kwa kiongozi wa upinzani Dkt Kizza Besigye mapema asubuhi.

No comments

Powered by Blogger.