Header Ads


MAASAI WAMFANYIA IBADA RAISI MAGUFULI


Zaidi ya viongozi mia moja wa mila kutoka kabila la maasai  kwenye  wilaya za watu wa jamii hiyo wamekusanyika wilayani monduli  kumisimika Kiongozi Mkuu   wa mila wa koo ya Ilikisongo  na kufanya ibada maalum ya kimila ya kumwomea Rais Magufuli na serikali yake  waendelee kupambana na wafujaji wa mali ya umma.
Katika tukio ilo lililohudhuriwa na viongozi wa mila kutoka wilaya za mikoa ya Arusha, Manyara, Morogoro na kwingineko  pamoja baadhi ya viongozi wa kisiasa  ambapo wengi wao ni wa jamii hiyo viongozi wa mila wamesema wapo tayari kushirikiana na serikali katika kuwafichua watendaji wazembe na wauza ardhi ya umma  ili kuwaondoa watanzania kwenye dimbwi la umasikini.
 
Kiongozi aliyesimikwa kama mwenyekiti wa viongozi wa mila wa koo hiyo Kibori Ngelipoi  akizungumza huku akitafsiriwa kwakuwa hajui lugha ya kiswahili amesema nafasi ya viongozi wa mila katika jamii ni kubwa naye  atahakikisha atatumia vizuri nafasi hiyo.
 
Baadhi ya viongozi wa kisiasa waliyo hudhuria tukio ilo wamewahasa viongozi wa mila kutochanganya siasa na mila kwakuwa  vitashusha ufanisi wao katika  kutatua masuala ya kijamii.

No comments

Powered by Blogger.