Watu 2 wamefariki na wengine kadhaa kunusurika baada ya mashua waliokuwa wakisafiria kuzama katika Ziwa Tanganyika.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kigoma kamishna msaidizi mwandamizi wa
polisi Ferdinand Mtui amesema mashua hiyo iliyokuwa na shehena ya mizigo
na abiria sita ilikumbwa na dhoruba katika eneo la Msulumbuka katika
pwani ya milima ya hifadhi ya Taifa ya mahale .
Amesema dhoruba hiyo ilisababisha mashua inayoiwa Salum Line
kugonga mwamba na kupasuka hali iliyosababisha mizigo yote kuzama na
watu wawili Pilila Ntagata na dada yake ambaye hajafahamika kufa huku
wengine wakifanikiwa kuogelea mpaka nchi kavu.
Kutokana na hali hiyo ametoa tahadhari kwa wananchi hususan wavuvi
na wanaoendesha shughuli za usafirishaji katika Ziwa Tanganyika
kuzingatia utabiri wa hali ya hewa na kuchukua tahadhari za kiusalama .
Post a Comment