Wavuvi zaidi ya 1000 wa kisiwa cha Kasarazi Mwaza wagoma kufanya kazi kupinga manyanyaso kutoka kwa wamiliki.

Zaidi
ya wavuvi 1,000 wa kisiwa cha Kasarazi wilaya ya Sengerema mkoani
mwanza,wamegoma kufanya kazi kwa siku ya nne mfululizo wakipinga vitendo
vya unyanyasaji,ikiwemo kunyimwa chakula vinavyodaiwa kufanywa na
wamiliki wa mitumbwi,huku uongozi wa serikali wilayani humo
ukilalamikiwa kwa kufumbia macho vitendo hivyo vinavyoweza kusababisha
uvunjifu wa amani.
Katibu wa umoja huo wa wavuvi wapatao 1,165 waliopo katika kisiwa
cha Kasarazi halmashauri ya wilaya ya Buchosa Boniphace Mgeta amesema
wameamua kugoma kuingia ziwani kuendelea na shughuli zao za uvuvi kwa
madai ya kunyanyaswa na matajiri hao,huku mkuu wa wilaya hiyo Zainab
Talack akishindwa kuupatia ufumbuzi mgogoro huo licha ya kukutana na
pande hizo mbili ofisini kwake .
Uongozi wa wamiliki wa vyombo vya uvuvi wa kisiwa hicho cha
Kasarazi kilichomo ndani ya Ziwa Victoria, kupitia kwa katibu wao
Msilikale Juma amesema chanzo cha mgogoro huo ulioanza kufukuta kuazia
mwezi Aprili mwaka huu ni hujuma inayodaiwa kufanywa na baadhi ya wavuvi
wasio waaminifu na kusababisha hasara ya mamilioni ya shilingi kwa
wamiliki wa vyombo vya uvuvi.
Mkuu wa wilaya ya Sengerema Zainab talack akizungumza na ITV kwa
njia ya simu kutokea wilayani Sengerema amekiri kuutambua mgogoro na
kuzitaka pande zote mbili kukaa chini na kufanya mazungumzo yenye lengo
la kufikia mwafaka.
Post a Comment