MABWANA NA MABIBI SHAMBA SASA NI MARUFUKU KUKAA OFISINI KILOLO
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilolo Bw Aloyce Kwezi akiwa na mkuu wa wilaya ya Kilolo Bi Asia Abdalah katika viwanja vya nane nane jijini Mbeya mara baada ya waziri mkuu kumaliza kufunga maonyesho hayo
Na MatukiodaimaBlog
SERIKALI ya wilaya ya Kilolo mkoani Iringa imewaagiza mabwana na mabibi shamba katika halmashauri hiyo kutoka maofisini na kwenda mashambani kuwasaidia wakulima kulima kisasa ili kuongeza uzalishaji wa mazao.
Mkuu wa wilaya ya Kilolo Bi Asia Abdalah aliyasema hayoa wakati wa kilele cha maonyesho ya wakulima (nane nane ) kwenye banda ya Halmashauri ya wilaya ya Kilolo wakati wa kufunga maonyesho hayo juzi.
Alisema kuwa pamoja na wilaya yake kuonyesha ushiriki mzuri wa maonyesho hayo na wananchi wengi kufika kujifunza katika banda la Kilolo namna ya kilimo bora chenye tija ila alisema bado wao kama Kilolo kwa kushirikiana na mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Bw , Aloyce Kwezi pamoja na wataalam wote hasa wale wa kilimo kufanya kazi kama timu ili kuwasaidia wakulima wa Kilolo kusonga mbele
Mkuu huyo alisema kuwa kati ya wilaya zinazoongoza kwa kilimo cha mahindi na mazao mengine ya biashara ndani ya mkoa wa Iringa ni pamoja na wilaya hiyo ya Kilolo hivyo alisema iwapo kila mtaalam wa kilimo atawajibika kwa nafasi yake kauli mbiu ya Rais Dr John Magufuli ya Hapa Kazi tu inaweza kuwasaidia wananchi kuongeza kasi ya uzalishaji .
Kwani alisema pamoja na jitihada kubwa zinazofanywa na wataalam hao wa kilimo katika wilaya ya Kilolo katika kuwasaidia wakulima ila bado zipo changamoto kiasi kwa baadhi ya wataalam wa kilimo kutotimiza wajibu wao .
“ Lengo ni kuona kila bwana shamba ama bibi shamba kwa maana ya wataalam wa ugani wote wanatimiza wajibu wao kwa kutoka maofisini na kwenda mashambani walikowakulima ili kuwasaidia kuongeza kasi ya uzalishaji zaidi”
Hata hivyo alisema iwapo wataalam wa kilimo watakwenda kwa wananchi na kushinda nao mashamani upo uwezekano wa wilaya ya Kilolo kwa maonyesho yajayo kushika nafasi ya kwanza kikanda na kuwa na wakulima wenye kasi kubwa ya uzalishaji .
Pia alisema moja kati ya majukumu ambayo yametolewa na waziri mkuu wakati wa ufungaji wa maonyesho hayo ni pamoja na kusimamia kasi ya uzalishaji na kuwa kwa wilaya ya Kilolo suala hilo linawezekana kusimamiwa na kufanikiwa kwa kiasi kikubwa .
Huku kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Kilolo Bw Aloyce Kwezi alisema kuwa wilaya hiyo iaongoza kwa kilimo cha nyanya ,vitunguu na mahindi pamoja na mazao mengine na kuwa uwezekano wa wananchi wa Kilolo kufanikiwa kiuchumi upo mkubwa iwapo kila mmoja atatimiza wajibu wake .
Alisema zao la nyanya limekuwa ni ukombozi mkubwa kwa wananchi wa Ilula kama ilivyo zao la vitunguu kwa waanchi wa Nyanzwa na kudai hadi sasa serikali imeendelea kuwasaidia wakulima hao katika kuboresha skimu za umwagiliaji katika maeneo ya Mtandika , Ruaha mbuyuni na Nyanzwa na kuwa kupitia skimu hizo wananchi wameweza kuongeza uzalishaji .
Post a Comment