Header Ads


KUCHAPWA VIBOKO 70 KWA ATAKAE HARIBU MAZINGIRA SIMANJIRO


Baada ya kukithiri kwa uharibifu wa mazingira  kwenye mito na vyanzo vya maji  uliyosababisha ukame katika kijiji cha Terati wilaya ya Simanjiro viongozi wa mila pamoja na serikali ya kijiji imeweka adhabu ya bakora sabini kwa mtu atakayeingiza mifugo kwenye maeneo hayo  adhabu ambayo inasemekana imeanza kufakisha  kukomesha tabia hiyo.
Wakizungumzia athari hizo baadhi ya viongozi wa mila na wakijamii wamesema imesababishwa na uelewa mdogo wananchi juu ya umuhimu wa vyanzo vya maji na tangu walipoanza kutoa adhabu ya kuchapwa bakora sabini kwa anayekutwa ameingiza mifugo kwenye mto au chanzo cha maji mazingira yameanza kurudi kwenye hali ya kawaida.
 
Mwenyekiti wa kijiji cha Terati Godson Nduya amekiri kuwa hali ya uharibifu imekuwa mbaya ukame umekithiri na kuchangia kudumaza maendelea ya jamii lakini mipango ya kunusuru inaendelea. 
 
Mkurugenzi wa mazingira ofisi ya makamu wa Rais Julias Ningu ambaye aliambatana na baadhi ya watalaam kujionea uharibifu huo amesema watalam wengi wamejitokeza kutekeleza miradi ya kuokoa mazingira lakini kumekuwa na urasimu mkubwa kwenye vyombo vya fedha unaofifisha juhudi za watalaam kuokoa mazingir

No comments

Powered by Blogger.