TANGA MARUFUKU KUKARIBISHA WAGENI
![]() |
Wakazi
wa wilaya ya Kilindi kwa kushirikiana na viongozi wa serikali za
vitongoji na vijiji wameonywa kuacha kukaribisha wageni katika maeneo
yao kwa sababu bado kuna viashiria vya kuwepo kwa vikundi vya uhalifu
ambavyo viliwahi kuanzisha vikosi vya uhalifu vilivyodiriki kuua baadhi
na askari huku mkuu wa kituo cha polisi akijeruhiwa vibaya kwa risasi.
Wakizungumza katika mkutano wa hadhara na wakazi wa kata ya Negero
iliyopo wilayani Kilindi mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama
wilayani Kilindi Selemani Liwowa pamoja na watendaji wake wa serikali,
wamesema hali ya kuwepo kwa vikundi hivyo vya uhalifu bado ipo kufuatia
kukamatwa kwa baadhi ya watuhumiwa wanaojihusisha na kazi kutengeneza
silaha za moto.
Hata hivyo baadhi ya raia wema waliounda vikosi vya kukabiliana na
uhalifu waliofanikisha kuwakamata baadhi ya watuhumiwa wanaotengeneza
silaha zinazotumika katika vitendo vya uhalifu, wameiomba serikali
kupitia jeshi lake kuimarisha ulinzi kwa sababu baadhi ya watuhumiwa
waliokamatwa na silaha na nguo za jeshi la wananchi wameweka visasi kwa
wananchi.
Kufuatia hatua hiyo, mkuu wa mkoa wa Tanga akizungumza na maafisa
watendaji na wenyeviti wa serikali za mitaa jijini Tanga amewataka
kuwafichua wageni wanaoingia katika maeneo yao na kwamba jeshi
limeongeza nguvu katika zoezi la kukabiliana na wageni waliopo katika
mapango ya Amboni ambao wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya uhalifu.
Post a Comment