WAFANYA KAZI WA VYOMBO VYA UTANGAZAJI WAASWA KUWAJIBIKA ILI KUONGEZA KASI YA MAFANIKIO
Mkurugenzi Mtendaji wa ITV/Radio One JOYCE MHAVILLE ametoa changamoto kwa wafanyakazi wa vyombo hvyo vya utangazaji kuwajibika kwa nafasi zao katika kuendeleza kasi ya mafanikio ya kampuni hiyo.
Amesema mafanikio ya sasa ya kampuni hiyo yametokana na juhudi za
wafanyakazi wake na kwamba katika kipindi hiki cha ushindani wa vyombo
vya utangazaji juhudi za ziada zilikuwa zinahitajika katika kuleta
ufanisi na kutafuta matangazo ambayo ndiyo chanzo kikubwa cha mapato
yake.
Bi JOYCE MHAVILLE alikuwa akizungumza kwenye sherehe ya mwaka kwa
ajili ya wafanyakazi wa ITV/Radio One pamoja na baadhi ya wawakilishi
wake wa mikoani na Visiwani.
Kwa kawaida baadhi ya wageni mashuhuri kualikwa kujumuika na
wafanyakazi wa ITV/Radio One na mwaka huu mwanamuziki ALI KIBA na
mwigizaji wa tathmiliya ya ISIDINGO SISA HEWANA MAARUFU KAMA SKUMBUZO
walikuwa miongoni mwa wageni hao.
Katika hatua nyingine Mwanahabari na Mtangazaji mkongwe Raifred
Masako wa ITV/Radio One ambaye ameamua kustaafu Kufanyakazi na ITV/Radio
One akapata fursa kuwaaga waliokua wafanyakazi wenzake na kuwapa siri
ya mafanikio katika kufanya kazi na watu.


Post a Comment